Pemba connect ni gazeti mtandao ambalo
lilianzishwa mnamo mwezi wa
3 , 2010.
Madhumuni Makuu:
1. Kuipasha dunia kuhusiana na matukio yanayotekea Zanzibar
2. Kuitangaza Zanzibar , kimataifa .
3. Kuleta mabadiliko katika ulimwengu wa habari na Mawasiliano
Madhumuni Makuu:
1. Kuipasha dunia kuhusiana na matukio yanayotekea Zanzibar
2. Kuitangaza Zanzibar , kimataifa .
3. Kuleta mabadiliko katika ulimwengu wa habari na Mawasiliano
Pemba
Connect
inaweza kupatikana kupitia www.pembaconnect.blogspot.com
Na Pemba Live ni mtandao ambao ulisajiliwa tarehe 16 January, 2015 kama jina la biashara chini ya sheria no: 168 ya
Zanzibar na kupatiwa usajili namba 25/2015
Madhumuni
Makuu:
1. Kutangaza/Kuorodhesha Biashara
zote zilizoko kisiwani Pemba, Tanzania kwa ujumla (yaani Business Directory)
2. Kutangaza nafasi za ajira popote
duniani zinapotokea.
3. Kupashana matukio muhimu
yanayotokea kisiwani Pemba
Na Pemba live inaweza kupatikana kupitia anuani ya www.pembalive.info
Baada ya kukaa vikao
tofauti vya Bodi ya Ushauri ya kampuni kwa lengo la kuboresha huduma na
kutafuta jina jipya la gazeti mtandao la Pemba Connect, Uongozi wa kampuni tumeamua
kuunganisha mitandao yetu hii miwili ya Pemba
Connect na Pemba Live na kuunda
kitu kimoja.
Hivyo leo tarehe
09/12/2017, Tunatangaza rasmi kwamba
“Pemba Connect itajulikana kama Pemba Live, na huduma zote zilizokuwa
zikitolewa na mitandao yetu hii zitapatikana kwa kupitia mtandao mmoja wa www.pembalive.info”
In Shaa Allah,
kwa upande wetu, Kampuni ya Moyo Media
tunaendelea kuboresha zaidi gazeti letu, wadau wetegemee mambo mazuri kama vile
kuwa na App ambayo itakuwezesha kusoma gazeti, na huduma zote kwa kupitia
smartphone yako, tablets, laptop yako n.k popote duniani.
Tunatanguliza
shukrani kwa wateja wetu na wadau wote,
Ahsanteni
Sana,
Mustafa Moyo,
Afisa Mtendaji Mkuu, Moyo Media
Co. Ltd
No comments:
Post a Comment