Moyo Media - Adz

Moyo Media - Adz

Saturday, December 9, 2017

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU GAZETI MTANDAO – PEMBA CONNECT



Pemba connect ni gazeti mtandao ambalo lilianzishwa mnamo  mwezi wa 3 , 2010.
Madhumuni Makuu:
1. Kuipasha dunia kuhusiana na matukio yanayotekea Zanzibar
2. Kuitangaza Zanzibar , kimataifa .
3. Kuleta mabadiliko katika ulimwengu wa habari na Mawasiliano
Pemba Connect inaweza kupatikana kupitia www.pembaconnect.blogspot.com

Na Pemba Live ni mtandao ambao ulisajiliwa tarehe 16 January, 2015 kama jina la biashara chini ya sheria no: 168 ya Zanzibar na kupatiwa usajili namba 25/2015
Madhumuni Makuu:
1.    Kutangaza/Kuorodhesha Biashara zote zilizoko kisiwani Pemba, Tanzania kwa ujumla (yaani Business Directory)
2.    Kutangaza nafasi za ajira popote duniani zinapotokea.
3.    Kupashana matukio muhimu yanayotokea kisiwani Pemba
Na Pemba live inaweza kupatikana kupitia anuani ya www.pembalive.info

Baada ya kukaa vikao tofauti vya Bodi ya Ushauri ya kampuni kwa lengo la kuboresha huduma na kutafuta jina jipya la gazeti mtandao la Pemba Connect, Uongozi wa kampuni tumeamua kuunganisha mitandao yetu hii miwili ya Pemba Connect na Pemba Live na kuunda kitu kimoja.

Hivyo leo tarehe 09/12/2017, Tunatangaza rasmi kwamba “Pemba Connect itajulikana kama Pemba Live, na huduma zote zilizokuwa zikitolewa na mitandao yetu hii zitapatikana kwa kupitia mtandao mmoja wa www.pembalive.info

In Shaa Allah, kwa upande wetu, Kampuni ya Moyo Media tunaendelea kuboresha zaidi gazeti letu, wadau wetegemee mambo mazuri kama vile kuwa na App ambayo itakuwezesha kusoma gazeti, na huduma zote kwa kupitia smartphone yako, tablets, laptop yako n.k popote duniani.


Tunatanguliza shukrani kwa wateja wetu na wadau wote,

Ahsanteni Sana,

Mustafa Moyo,
Afisa Mtendaji Mkuu, Moyo Media Co. Ltd
 

No comments: